Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

WARAKA WA TUNDU LISSU KABLA HAJAKAMATWA NA POLISI TENA LEO

ZIKIWA zimebaki siku mbili ili kufanyika uchaguzi wa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, ambaye pia ni miongoni mwa wagombea nafasi ya Urais kwenye chama hicho, Tundu Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi asubuhi hii nyumbani kwake na kupelekwa katika Ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma.
==>Huu ni Ujumbe wa Tundu Lissu alioutumia mtandaoni
Wandugu wapendwa. Ninaandika haya nikiwa nyumbani kwangu Dodoma. Najiandaa kwenda mahakamani kwa ajili ya uamuzi wa Mahakama Kuu juu ya kesi ya kutaka kuzuia Uchaguzi wa TLS.
Ninawapa taarifa kwamba nimefuatwa nyumbani na askari wawili kutoka ofisi ya RPC Dodoma. Sijazungumza nao bado lakini ni wazi wana maagizo ya kunikamata na kunizuia kuja Arusha kwenye Uchaguzi wa TLS. Wameshindwa kuzuia uchaguzi wetu mahakamani…….
Wito wangu kwenu mawakili wa Tanzania:
Nendeni Arusha mkachague viongozi wa TLS watakaopigania haki za binadamu, utawala wa sheria na demokrasia. Msipofanya hivyo hakuna mtu yeyote, hata ninyi mawakili, atakayepona kwenye……..
Kumbuka, kama Nimrod Mkono anaweza kufungiwa ofisi na TRA ni wakili gani mwingine aliye salama???
Kama wakili anaweza kukamatwa mahakamani kwa kufanya kazi yake ya uwakili, ni nani miongoni mwetu aliye salama???
Nendeni mkapige kura kukataa mfumo wa aina hii.
Mimi naenda mahabusu, na pengine, gerezani. Nawaombeni kura zenu ili niweze kuwaongoza katika kipindi hiki kigumu.
Hiki sio kipindi cha kuwa na viongozi wanaojipendekeza kwa wanaokandamiza haki za watu wetu na haki za mawakili wetu.
Hiki ni kipindi cha kuwa na viongozi watakaopigania haki zenu na haki za watu wetu. Mnanifahamu. Nipeni jukumu hili la kuwaongoza kwenye giza hili nene. Msikubali kuyumbishwa.
Na wachagueni pia Makamu wa Rais, Mweka Hazina wajumbe wa Governing Council watakaokuwa na msimamo kama wa kwangu.
Nawatakieni kila la kheri. I’ll think of you all wherever they’ll take me to, wherever I’ll be incarcerated. This too shall pass. The race of man shall rise again. It always has. Nimemwambia na mke wangu naye aende Arusha akapige kura. So, everybody to Arusha. Go vote your consciences.
All the best.
TL

HII HAPA NGOMA YA NURUELI - TAUSI KAMA HUJAIONA

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top