MSANII maarufu wa filamu nchini Tanzania Irene Uwoya amefunguka na kuweka wazi juu ya tetesi zinazoendelea kuenea mtaani kuhusu kuolewa na msanii wa muziki wa bongo fleva Dogo Janja na kusema ni kweli kabisa ameolewa na msanii huyo kwani ndiye mwanaume wa ndoto yake.
“Nimeolewa na mwanaume wa ndoto zangu, bado naendelea kulia na kutokwa na machozi ya kwa furaha. Dogo Janja nakupenda sana na nimefurahi kumaliza maisha yangu ya duniani nikiwa na wewe” aliandika Irene Uwoya. katika ukurasa wake wa Instagram
Kufuatia ujumbe huu aliouandika Irene uwoya katika ukurasa wake wa Instagram, ni wazi kuwa Irene Uwoya atakuwa amejibu maswali ya watu wengi ambao walikuwa hawaelewi nini kinaendelea kufuatia tetesi kuwa watu hao wamefunga ndoa siku za karibuni.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.