Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

YANGA YAMTOA CHIRWA KWA MKOPO... YASAJILI MBADALA...

Klabu ya Yanga imemtoa kwa mkopo mshambuliaji wake raia wa Zambia Obrey Chirwa kwenda katika klabu ya Platinum ya Zimbabwe.
Taarifa kutoka ndani ya klabu Yanga imesema kuwa makubaliano hayo yalifikiwa dakika chache kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa usiku wa saa 5:59 siku ya jana (Desemba 15, 2016)
Taarifa hizo zimebainisha kuwa klabu hiyo imemsajili straika kutoka katika klabu ya Zesco, anayefahamika kwa jina
Winston Kalengo kama mbadala wa Chirwa.
Kwa mujibu wa makubaliano katika mkopo huo, Yanga itakuwa ikimlipa Chirwa nusu mshahara, na nusu nyingine itakuwa ikilipwa na Platinum.
Chirwa ni miongoni mwa wachezaji waliosajiliwa kwa kishindo katika klabu hiyo, ikidaiwa kuwa ndiye aliyekuwa mchezaji ghali zaidi akisajiliwa kwa dau la shilingi za kitanzania milioni 240, lakini hakuwa na mwanzo mzuri katika ligi kuu Tanzania Bara licha ya kuanza kufunga katika michezo ya mwisho ya mzunguko wa kwanza.
Hadi anaondoka klabuni hapo ameifungia mabao matano.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top