Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

CCM YAWASHUKURU WATANZANIA KWA USHIDI WA UBUNGE, UDIWANI...

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewashukuru Watanzania kwa kukipa ushindi katika uchaguzi wa ubunge wa Jimbo la Dimani, Unguja, na  udiwani katika kata nyingi  uliofanyika Jumapili iliyopita.
Hayo yalisemwa na Katibu  wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM,  Humphrey Polepole, alipozungumza na wanahabari leo katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.
Polepole alisema kwamba mchawi wa kushindwa kwa mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) yuko ndani ya chama hicho na kisitafute kisingizio kingine.
Mgombea wa CCM huko Dimani alishinda ambapo pia chama hicho kilishinda katika kata 19 kati ya 20 ambapo moja imechukuliwa na upinzani.
“Nawashukuru sana wananchi kwa kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi na  ujio wake mpya wa Hapa Kazi Tu chini ya Mwenyekiti wake, Rais John Pombe Magufuli na hivyo vyama vingine vitaendelea kukifuata chama hicho kwa nyuma,” alisisitiza katibu huyo.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top