Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

MKALIMANI AKAMATWA KUTAFSIRI UONGO MATAMSHI YA MTALII...

Mkalimani katika mbuga ya wanyama pori nchini Tanzania amekamatwa baada ya kutafsiri visivyo matamshi ya mtalii mmoja kuhusu nchi na watu wake.
Kwenye video iliyosambazwa kwa wingi, mkalimani huyo anasema kuwa mtalii huyo anataka watu wa Tanzania waache kulalamika kwa sababu ya njaa
Ukweli ni kwamba mwananke huyo anasema kuwa wata wa Tanzania ni wazuri kupindukia.
Alikamatwa siku ya Alhamisi kwa agizo la waziri wa utalii.
Mkalimani huyo ambaye hakutajwa jina ni kutoka mbuga ya Serengeti iliyo kaskazini magharibi mwa nchi.
Kamanda wa polisi eneo hilo Philipo Kalangi, aliiambai BBC kuwa anahojiwa lakini hakutoa habari za kina.
Mwandishi wa BBC mjini Dar es Salaam anasema kuwa huenda waziri alihisi kuwa mkalimani huyo alikuwa akimsuta mtalii au alikuwa akimuiga Rais John Magufuli.
Video hiyo iliyochapishwa na gazeti la Kenya, mtalii anasema:
"Hi. Ziara yangu nchini Tanzania imekuwa nzuri. watu ni wazui na wenye urafiki. Salamu kwa kawaida ni Jambo, nina furaha kuwa hapa, Ardhi ni nzuri."
Mkalimani anatafsiri hivi:
"Anasema watanzania mnalia sana njaa, kila siku mnalia nja wakati mna maua nyumbani, si mchemshe maua mnywe, anasema si vizuri kulia njaa."
Mtalii
"Aina nyingi ya wanyama na watu unaona ni wazuri, kinyume na sehemu zingine. Ni nzuri."
Mkalimani
"Anasema mnamuomba rais wenu awapikie chakula, kwani rais wenu ni mpishi, angahikeni mfanye kazi,chemsheni hata nguo mnywe."
Mtalii
"Ni kitu mabacho utakikumbuka katika maisha yako yote. Ni nzuri na ni ya kupendeza."
Mkalimani
"Anasema mhangaikeni pembezoni za nchi, muache rais hawezi kutoka Ikulu akuje kuwapikia chakula, hivyo mjipikie wenyewe."

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top