Manchester United wameshindwa kuondoka na ushindi ugenini dhidi ya Anderlecht baada ya kulazimishwa suluhu ya 1-1 katika hatua ya robo fainali.
Henrikh Mkhitaryan alianza kuiandikia bao United baada ya kazi nzuri ya Marcus Rashford Hii ikiwa ni dakika ya 37.
Kipindi cha kwanza Manchester United ilikwenda mapumzikoni ikiwa kifua mbele kwa goli 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikishambulia lango la mwenzake.
United ikiamini imemaliza kazi dakika ya 87 Leander Dendoncker akaiandikia Anderlecht goli la kusawazisha na kuhitimisha mchezo huo.
Marudio ya mchezo huu ni wiki ijayo na zamu hii United itakuwa nyumbani Old Trafford.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.