Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

MKUTANO WA CUF WAVAMIWA NA WATU WENYE SILAHA...



Watu wasiojulikana wakiwa na bastola wamevamia mkutano wa wanachama wa CUF ambao unamuunga mkono, Mwenyekiti wa Chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba na kushusha kipigo kwa baadhi ya wananchama wa CUF na waandishi wa habari.



Mkutano huo ambao ulikuwa na lengo la kumtambulisha Katibu Mkuu wa CUF, inadaiwa watu hao waliovamia mkutano huo na kufanya vurugu ni wanachama wa Cuf ambao wanamuunga mkono Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.
Kwa mujibu wa taarifa zilizokuwepo mkutano huo ulipangwa kufanyika majira ya saa tano za asubuhi katika hoteli ya Vina, Mabibo lakini kabla ya kuanza waliibuka watu hao wasiojulikana wakiwa wamevalia soksi nyeusi usoni kuficha sura zao na kushusha kipigo kwa baadhi ya wanachama wa CUF waliokuwepo katika eneo hilo na waandishi wa habari.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top