MSANII wa Bongo Fleva nchini Abelnego Damian, ‘Belle9’, amepata pigo baada ya kuondokewa na baba yake mzazi Damian Nyamoga.
Meneja wa Belle9, Jahz Zamba amethibitisha taarifa hiyo huku akieleza kuwa mzee Damian amefariki dunia kwa kugongwa na bodaboda iliyokuwa kwenye mwendo mkali huko mjini Morogoro ambako alilikuwa akiishi.
Jahz amfunguka kuwa ni pigo kubwa kwa Belle 9 kumpoteza baba yake kwa kuwa mara nyingi amekuwa akidai kuwa baba yake ni mwalimu muhimu katika maisha yake. Staa huyo anayetokea Morogoro amelikuwa na mahusiano mazuri na baba yake kama mtu na rafiki yake.
Msiba Upo nyumbani kwa marehemu Morogoro mjini alipokuwa akiishi.
Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi "ameen"
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.