Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

SHUGUDIA HAPA MOTO MKALI ALIOWASHA ISAYA MSANGI MWANZA



Mwimbaji wa Nyimbo za injili Nchini Tanzania Isaya Msangi, amefanya kufuru katika ibada za Jumapili alizokaribishwa kuhudumu huko Jijini Mwanza katika kanisa la Ukombozi na kuwafanya waumini kupagawa kwa nyimbo zake mbili mpya alizoimba.

Akizungumza na Gospel 1 Magazine Isaya Msangi Ambaye pia ni daktari wa maginjwa ya binaadamu, amesema kuwa hakutegemea mapokeo ya kiasi hicho kwani nyimbo hizo ni mpya na hazina promo bado, lakini ameshangazwa na jinsi watu walivyozipokea nyimbo hizo kwani watu hawakutaka hata kukaa chini.

"... hakika nimeuona mkono wa Mungu katika ujio wa Nyimbo zangu hizi imbili ambazo nilikuwa bado sijazitambulisha rasmi, lakini kwa moto ulivyowaka pale Mwanza kusema ukweli, mkono wa Mungu uko juu yangu... naamini kabisa nyimbo hizi zitakuja kuwa kuja moto wa kuotea mbali..."

Isaya amewasha moto huo katika kanisa la Ukombozi chini ya Mchungaji BG Malisa Jijini Mwanza - Tanzania ambapo aliimba nyimbo zake mpya Kimeeleweka na Leo ni Zamu Yako.

TAZAMA VIDEO HAPA

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top