Mechi ya Arsenal dhidi ya Cologne katiika kombe la Yuropa ilikumbwa na ghasia na kusababisha kucheleweshwa kwa saa moja.
Maelfu ya mashabiki wa kigeni waliwasili katika uwanja huo bila tiketi na kulikuwa na ghasia kati ya mashabiki na wapokezi wao ndani ya uwanja huo baada ya mlango kufunguliwa.
Maafisa wa polisi walisema kuwa watu watano walikamatwa kwa tuhuma za kuhusika katika ghasia.
Kulikuwa hakuna ripoti zozote za ghasia wakati wa mechi hiyo ambayo Arsenal ilishinda magoli 3-1.
Timu hiyo ya Ujerumani ilikuwa imepewa tiketi 2,900 pekee.
Lakini takriban mashabiki 20,000 wa timu hiyo waliingia na kusimamisha biashara mjini London nyakati za mchana Alhamisi.
Hatahivyo hivyo mechi hiyo ilianza baada ya kucheleweshwa kwa saa moja.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.