
Msanii wa kizazi kibya Harmonize na Msanii wa Filam Jacklin Wolper
Ikiwa maneno mengi yakiwa yanaendelea kusemwa kwenye midomo ya baadhi ya watu na baadhi ya vyombo vya habari ikiwemo na mitandao ya kijamii kuhusu penzi la mwanamuziki wa kizazi kipya Harmonize na msanii wa Bongo Movie Jackline Wolper kuwa hawaendani, Mbongo flava huyo ameamuakutupia picha hii kwenye ukurasa wake wa fb na huku akitupia maneno haya.
"...Mimi nakupenda sitokutenda wanasema mengi maneno mengi ila hayatojenga..."
Kauli inaonesha kuwa Harmonize alitaka kuwakata ngebe wale wote wanaolidisi penzi lao na wanaosema kuwa Wolpe anambemeda.
Penzi la wawili hawa lilianza kimya kimya lakini kadri siku zilivyozidi kwenda likaenda linachipua mpaka kuwa hadharani na kuzaa minongono kwa watu ambayo nayo haikujificha ikawa hadharani kuwa Wolper na Harmonize hawaendani kutokana na kuwa Wolpe anaonekana mkubwa kwa Harmonize... lakini wao wanaamini kuwa penzi halichagui mkubwa wala mdogo na ndio maana penzi lao linachipua kila kukicha.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.