Wabunge wote wa vyama vya upinzani leo tena wametoka nje kupinga Naibu Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson kuendesha vikao vya Bunge huku wakisema wanamwachia Bunge yeye na wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Taarifa kutoka Bungeni zinaeleza kuwa, wabunge wote wa upinzani wametoka nje kususia kikao cha Bunge ikiwa ni kutekeleza azimio lao la kutokuwa na imani na Naibu Spika, Dk. Tulia.
Baada tu ya kusomwa dua ya kufungua Bunge, wabunge hao wametoka nje majira ya saa 3:00 asubuhi na kumwacha Dk. Tulia akiwa na wabunge wa CCM pekee.
Kambi upinzani ilianza utaratibu huo juzi kwa kutoka ndani ya ukumbi wa Bunge baada ya Dk. Ackson kuingia ukumbini.
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, juzi alisema wataendelea kutoshiriki vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika hadi pale “haki itakapopatikana.”
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.