Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Josephat Gwajima jana July 12 2016 amekamatwa na polisi wakati anawasili Tanzania kutokea ughaibuni ambapo baada ya kukamatwa alichukuliwa na kuhojiwa kwa saa kadhaa kituoni.
Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro amesema Gwajima amehojiwa kutokana na kauli yake ya uchochezi aliyoitoa kabla hajasafiri kwenda nje ya nchi. kamanda sirro amesema kuwa tayari walishamuhoji na upelelezi unaendelea.
‘Alipofika tu uwanja wa ndege alichukuliwa, yeye alifikiri anaweza tu kuja kimyakimya bila kuonekana…. uwezekano wa kutoonekana ni mdogo sana, tumeshamuhoji vizuri upelelezi unaendelea na tukipata ushahidi wa kutosha sheria itachukua mkondo wake, yuko nje kwa dhamana‘ – alisema Sirro.
‘Alipofika tu uwanja wa ndege alichukuliwa, yeye alifikiri anaweza tu kuja kimyakimya bila kuonekana…. uwezekano wa kutoonekana ni mdogo sana, tumeshamuhoji vizuri upelelezi unaendelea na tukipata ushahidi wa kutosha sheria itachukua mkondo wake, yuko nje kwa dhamana‘ – alisema Sirro.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.