DAR ES SALAAM: Sehemu ya Kituo cha Mafuta cha Gapco kilichopo eneo la Kamata jijini Dar es Salaam, kimebomolewa mapema leo kwa kile kilichoelezwa kuwa kituo hicho kipo ndani ya eneo la reli Tanznia (TRL).
Zoezi hilo la bomoabomoa ambalo limeanza asubuhi ya leo, limeendeshwa na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) dhidi ya watu waliofanya maendelezo ya ujenzi ndani ya eneo la reli hiyo.
Sehemu ya kituo hicho cha mafuta cha gapco, kilibomolewa na kuwaacha wafanyakazi na baadhi ya watu waliokuwa maeneo ya jirani kulishangaa tukio hilo ambalo halikutarajiwa kuwa litafanyika leo.
KAMA HUJABAHATIKA KUSIKILIZA WIMBO MPYA WA DAMU TULIZA MOYO, HUU HAPA
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.