MKUU wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda leo Machi 29, amebanwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo hivi punde ameanza kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ili kujibu tuhuma zinazomkabili.
Hatua hiyo ya kumita RC Makonda kujibu tuhuma zinazomkabili ilifikiwa bungeni wiki chache zilizopita baada ya kuafikiwa kwa hoja iliyotolewa bungeni na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara, kufuatia kauli inayodaiwa kutolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda inayodaiwa kuwa ni dharau kwa Bunge.
Pia Mwita alidai kuwa viongozi mbalimbali hasa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wamekuwa wakitumia madaraka yao vibaya kiasi cha kuingilia majukumu yasiyo yao, na wakati mwingine kuingilia majukumu ya Bunge, na kutolea mfano Paul Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Alexander Mnyeti.
tutaendelea kuwajuza kinachoendelea.
WENGI WANASEMA UNAFANANA NA MOYO SUKUMA DAMU... SIKILIZA MWENYEWE,,,
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.