Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

ALIYOYASEMA NAUYE LEO DHIDI YA RAIS MAGUFULI...

Aliyekuwa waziri wa habari, utamaduni, Sanaa na michezo nchini Tanzania Nape Nnauye amesema bado anaunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kujaribu kufanikisha mageuzi nchini humo.
Bw Nnauye, akizungumza wakati wa kukabidhi rasmi afisi kwa mrithi wake Dkt Harrison Mwakyembe, kadhalika amesema ataendelea kushirikiana na wizara hiyo.
Amesema yeye ni mdau mkubwa katika sekta zilizomo chini ya wizara hiyo.
Bw Nnauye alifutwa kazi wiki iliyopita siku moja baada yake kupokea ripoti ya kamati ya uchunguzi kuhusu uvamizi uliotekelezwa na mtu anayedaiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda katika studio za kituo cha habari cha kibinafsi cha Clouds.
Kamati hiyo, kwenye ripoti yake, ilionekana kumkosoa Bw Makonda na kusema alitumia vibaya mamlaka yake.
"Heshima aliyonipa mheshimiwa Rais ni kubwa mno na nitaendelea kumuunga mkono katika dhamira yake njema ya kuleta mageuzi nchini," alisema Bw Nnauye, kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wizara ya habari na michezo Tanzania.
Taarifa hiyo inasema Bw Nnauye ameahidi ataendelea kuwa mtiifu kwa Rais Magufuli, serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Bw Nnauye, ambaye ni mbunge wa Mtama, alisimamia wizara hiyo kwa miezi 15.
Waziri mpya Dkt Mwakyembe amesema anategemea kuendelea kupata ushirikiano kutoka kwa Bw Nnauye.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top