Mwanamuziki wa
Kizazi kipya anayechipukia kwa kasi anayefahamika kwa jina la Chaka Yes
ambaye ni ndugu wa Harmorapa yuko tayari kuachia ngoma yake mpya
aliyofanya katika studio za Combination
Sound chini ya Producer Man Walter.
Akizungumza na
MO Design, Mwanamuziki huyo
aliyefahamika zamani kwa jina la Chaka Mlingula, amaesema kuwa Wimbo huo uitwao SALAM
aliimba kwa kushirikiana na Producer huyo mwenye mbwembwe katika uimbaji Man Walter.
Kabla ya
ngoma hiyo, Chaka Yes aliwahi
kutamba na Ngoma inayokwenda kwa jina la Sidhani kama ntapendwa ambayo ilifanya vizuri
katika vyombo mbali mbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii. Ngoma hiyo
bado inaendelea kufanya vizuri ikiwa katika mfumo wa Audio na Video.
“ naachia kwanza ngoma
hii ya Salam ikiwa ni audio tu, napenda mashabiki zangu waizowee kwanza ikiwemo
na kunipamaoni na ushauri wao kabla sijafanya video” alisema Chaka,
“… unajua siku zote
bila kupata maoni na ushauri wa watu wanaokufanya uendelee kuwa katika nafasi
uliyopo, huwezi kufanya vizuri… so lazima nipate maoni ikiwemo na Baraka zao
pia…” alimalizia
chaka huku akicheka.
Chaka
alisema ataanza maandalizi ya video baada ya kupata maoni kutoka kwa mashabi wake,
kwani hapendi tena kufanya video itakayokuwa ya kawaida bali tu, anataka afanye
video itakayowafanya mashabiki wa Harmonise
wahamie kwake.
Alipoulizwa kwa
nini anataka mashabiki wa Harmonise, akasema kuwa kiuwezo yeye ni zaidi ya
Harmonise, kwanini msani huyo awe na mashabiki zaidi yake?.. So anataka kufanya
kitu kitakachowaleta wale walioko kwa Harmonise warudi kwake kwani anaamini
wote ni wa kwake lakini wako kule kwa vile walikuwa hawajamsikiliza vizuri yeye.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.