![]() |
| ASHA ZULU MANDELA |
Siku zote nasema ukichelewa kufa utaona mengi... Dada huyu ndiye anayeshikilia rekodi ya dunia ya binaadamu mwenye Rasta ndefu kuliko wote.
Asha Zulu Mandela anashikilia rekodi ya World Guiness Book ya Binaadamu mwenye rasta ndefu kuliko wote duniani kote.
Asha Zulu Mandela, alizaliwa katika visiwa pacha vya Trinidad na Tobago, na baba yake Asha ni mwenyeasili ya South Afrika.
Asha anasema alipoanza kufuga Rasta zake, hakuwa na uhakika kama zitakuwa, kwani hata mama yake alikuwa akimpiga vita kuhusu ufugaji wa aina hiyo ya nywele.
Asha anasema kuwa pamoja na vikwazo vya mama yake aliyekuwa akimuambia kuwa, kuwa na aina hiyo ya nywele ni uhuni na uchafu, lakini hakukata tamaa na aliendelea kufuga na kuzipa matunzo mazuri mpaka sasa anashikilia rekodi ya dunia ya mtu mwenye Rasta ndefu kuliko wote.
Endelea kufuatilia modesigntz Beste wangu wa ukweli,na mimi ntaendelea kukuleteakila story inayonifikia...
PIA USISAHAU KU LIKE PAGE YETU ILI NA WEWE UWE MWANAFAMILIA NA HABARI ZETU ZIWE ZINAKUFIKIA MOJA KWA MOJA...
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN



Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.