Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

HII NI KWA AKINA DADA MNAOPENDA KUVAA SURUALI ZA KUBANA...ONA ATHARI ILIYOMKUTA DADA HUYU...

skinny-jeans-for-women


Kama wewe ni mtu wa fashion na style za kisasa kwenye ishu ya mavazi, basi hii stori iwe karibu na wewe…
fasion za mtu kuvaa nguo za kubana hua zipo tu siku zote, lakini umeipata stori ya Australia kilichomkuta mtu aliyevaa suruali yakubana?..

Ripoti kutoka Australia inahusu ishu ya mwanamke mmoja kulazwa Hospitali kwa muda wa kama siku nne hivi, kutokana na mishipa yake kupata majeraha baada ya kuvaa nguo ya kubana alafu akachuchumaa kwa muda mrefu.

Mwanamke huyo  alijisikia kama ganzi hivi alipoinuka, akajaribu kutembea lakini hakufika mbali.. alianguka na baada ya muda kidogo alipata msaada wa kufikishwa Hospitali.

Dr. Thomas Kimber ni daktari katika Hospitali ya Royal Adelaide, Australia ambapo mwanamke huyo alipelekwa kutibiwa… Dokta anasema alishangazwa na jinsi ambavyo mgonjwa huyo alipata majeraha hayo yaliyotokana na nguo aliyoivaa.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top