Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

UKAWA WAIZUNGUMZIA AFYA YA EDWARD 1LOWASSA...

lowassa
KUFUATIA kuwepo kwa minong’ono juu ya afya ya mgombea urais wa Tanzania kupitia umoja wa vyama unaounda Ukawa, Edward Lowassa, umoja huo umetoa ufafanuzi na kusema kiongozi huyo yupo fiti kiafya.
Jumanne wiki hii baada ya waandishi wa habari kuzuiwa kuingia katika chumba cha kuchukua fomu kwenye Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dar kwa kile ambacho viongozi wa Ukawa walisema ni ukosefu wa hewa kutokana na udogo wa chumba, ilianza minong’ono kuwa afya ya Lowassa labda siyo.
Lakini Ofisa Habari wa Chama cha Wananchi (Cuf), Silas Bwire alipoulizwa juu ya hilo alisema madai hayo ni propaganda za wapinzani wao kisiasa kwani afya ya kiongozi huyo iko vizuri.
“Kwanza watu wanatakiwa wajue afya si mali ya mwanadamu, ni mali ya Mungu, binadamu haupaswi kumhukumu mwenzako kuhusu afya yake, wakati wewe mwenyewe hujajua kitu gani kinatokota tumboni mwako,” alisema Bwire.
Alisema Lowassa ana afya nzuri ndiyo maana anaendelea na mapambano ya kwenda ikulu.
Wakati huohuo, Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, Salum Mwalimu alisema hali ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe aliyefikishwa hospitali hapo Jumatatu ya wiki hii imeimarika na kwamba tatizo lake lilisababishwa na uchovu tu

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top