Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

ASILI NA LUGHA YAO YA LINGALA, IMECHANGIA MAFANIKIO YAO... LUKAKU NA YANNICK BOLASIE

Wachezaji wa Everton Romelu Lukaku na Yannick Bolasie, ambao wametajwa kuwa washambuliaji walio na ushirikiano mkubwa zaidi, wakiwa wamefunga mabao manane kwa kushirikiana msimu huu, wamefichua kuwa asili yao ambayo ni Jamhuri ya Demokrasi ya Congo ndiyo imechangia mafanikio yao.
Bolasie aliambia gazeti la Liverpool Echo kuwa, wao huwasiliana kwa lugha ya Lingala ili kuwachanganya walinzi ambao wanajaribu kupima mienendo yao.
"Hamna walinzi wengi wanaofahamu lugha ya Lingala kwa hivyo hilo hutupatia fursa nzuri," alisema Bolassie.
Lukalu ni raia wa Ubelgiji lakini wazazi wake ni raia wa Congo huku Bolasie huchezea timua ya taifa ya Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Huu ni mfano wa lugha ambayo wachezaji hao hutumia uwanjani jinsi ivyotafsiriwa na Mila Kimbuni kutoka Jamhuri ya Demokrasi ya Congo ambapo lugha hiyo hutumiwa sana.
Weka mpira eneo la hatarai - "Tinda N'ango cote oyo!"
Weka kwa kichwa- "Mutu"
Songa mbele- "Landa nzela"
Shambulia- "Marquer nbala moko"
Moja mbili- "Zongisela Nga Ango"

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top