Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

HII HAPA YA MKENYA ALIYESHINDA KITI CHA USENETA AUTRALIA...

Mwanamke mmoja mzaliwa wa Kenya Lucy Gichuhi, anatazamiwa kuwa mtu wa kwanza mwenye asili ya kiafrika kuketi kwenye baraza la bunge la seneti lenye waakilishi 76, ikiwa uteuzi wake utathibitishwa na mahakama kuu, gazeti la The Guardian limeripoti.
Bunge la Seneti la Australia, lina nguvu ya kurekebisha au kumtimua mbunge.
Alipata kiti hicho baada ya mwenzake kutoka chama cha Family First -FF, Bw Bob Day, ambaye awali alishinda kwenye uchaguzi, kulazimishwa kuachia kiti hicho.
Bi Gichuhi, ambaye ni mhasibu na wakili, alihamia Australia mnamo mwaka 1999 na akapata uraia wa nchi hiyo miaka miwili baadaye, hii ni kwa mjibu wa taarifa kutoka kwa runinga ya ABC.
ABC imemnukuu akisema:
"Ninashukuru kwa heshima kubwa kwa kupewa nafasi hii ya kuwatumikia wa-Australia....ninalichukulia kama fursa kubwa ya kulitumikia taifa hili kubwa."
Tangazo la mtandaoni, kwamba angekabiliwa na upinzani ikiwa ingebainika wakati fulani kuwa ana uraia wa mataifa mawili, lakini alisema kuwa "ana haki ya kutumikia".

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top