Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

SOMA HALI INAVYOENDELEA NCHINI BURUNDI, WANAJESHI HUSHANGILIWA KILA WANAPOONEKANA...


Hali ya amani nchini Burundi bado si shwari baada ya Rais kupinduliwa na jeshi la nchi hiyo, kwa madai ya rais huyo kutaka kugombea urais kwa mara ya tatu tena.
Rais huyo ameshindwa kurejea nchini mwake kutoka katika mkutano wa Viongozi wa kanda,baada ya ndege yake kugeuza kurejea ilikotokea.

 Ingawa askari watiifu kwa rais huyo wamedai kuzima jaribio hilo la mapinduzi yaliyokuwa yakiongozwa na meja jenerali Godefroid Niyombare dhidi ya rais wao,na kwamba udhibiti wa nchi uko mikononi mwao na hasa katika maeneo muhimu ya mji mkuu wa nchi hiyo ,Bujumbura.
Makabiliano ya risasi yamesikika karibu na vituo vya redio na runinga .mwandishi wa BBC aliyeko nchini Burundi amesema kwamba ameshuhudia jeshi likiwa limegawanyika pande mbili ,na haijulikani nani ameshikilia udhibiti wa nchi kwa sasa.
lakini pia wananchi wa nchi hiyo wamesema kwamba wao hawana tazizo na jeshi na ndio maana kila wanapowaona huwashangilia kwani lengo lao ni kutaka kuleta amani katika nchi.
Rais Nkurunziza amekosolewa kwa haja yake ya kuwania muhula wa tatu wa uongozi nchini Burundi, maamuzi ambayo yalisababisha wiki kadhaa za maandamano ambapo watu ishirini wameripotiwa kupoteza maisha.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top