

(PICHA: DENIS MTIMA/GPL)
Chama cha Wananchi (CUF) kimesema hakitakubali kurudia uchaguzi wa urais visiwani Zanzibar.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa chama hicho ambaye pia alikuwa mgombea wa urais katika uchaguzi wa Oktoba 25, 2015, Maalim Seif Sharif Hamad amesema hakuna hoja wala msingi wa kikatiba na kisheria wa uchaguzi wa Zanzbar kurudiwa na kufanya hivyo ni kuhalalisha vitendo vilivyofanywa na Tume ambavyo vimekiuka katiba.
Maalim Seif ameongeza kuwa subira ya Wanzibar izae haki ili kuepusha machafuko na migogoro ambayo inaweza kujitokeza kutokana na Uchaguzi wa Zanzibar kufutwa na mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi kinyume na sheria na katiba ya uchaguzi kwa shinikizo la viongozi wachache na kwa maslahi ya chama kimoja.
Aidha Maalim Seif amemtaka aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ZEC, Salimu Jecha kujiuzulu kwa kuwa alitangaza matokeo kinyume kwa madai ya kuwa na mapungufu.
Mbali na hayo ametaja vipengele vingi vya katiba ambavyo vinaainisha ukiukwaji mkubwa wa uchaguzi huo
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Filed Under:
Siasa
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.