WANAWAKE wakazi wa mji wa Kigoma, wamekumbwa na taharuki kufuatia kuibuka kwa mtu asiyefahamika anayewaingilia kinguvu wakati wa usiku wakiwa wamelala kwenye nyumba zao huku akitumia panga kuwatisha au kuwakatakata mapanga sehemu mbali mbali za miili yao wale wanaokataa kutekeleza matakwa yake.
Mpaka sasa zaidi ya wanawake 10 wanaelezwa kuvamiwa na mtu huyo ambaye kwa sasa ni maarufu kwa jina la Teleza, na inadaiwa kuwa huwafuata Zaidi wanawake wasio na waume na hutumia kisu kuharibu vitasa vya milango kabla ya kuingia ndani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Ferdinand Mtui, amethibitisha taarifa za matukio hayo huku akieleza kuwa tayari mtu mmoja amekamatwa na anaendelea kuhojiwa
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN

Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.