Nigeria imetangaza kwamba itauza ndege mbili zinazotumiwa na rais wa nchi hiyo kama njia ya kupunguza matumizi mabaya ya pesa za umma.
Msemaji wa Rais Muhammadu Buhari, Garba Shehu, amesema ndege hizo mbili kati ya 10 zinazotumiwa na rais wa nchi hiyo zitauzwa kama sehemu ya kupunguza 'ubadhirifu' wa serikalini.
Serikali imeweka tangazo magazetini kwamba inauza ndege hizo, moja aina ya Falcon 7X na nyingine Hawker 4000.
- Rais Buhari awataka Wanigeria wabadili tabia
Bw Shehu amesema Rais Buhari ndiye aliyeidhinisha matangazo hayo.
Ameongeza kwamba baadhi ya ndege nyingine za rais zitakabidhiwa jeshi la wanahewa la nchi hiyo.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.