Welcome

    Featured Posts

    MO DESIGN

    Social Icons

Loading...

NIGERIA YANADI NDEGE ZAKE KUKABILIANA NA UBADHILIFU



Rais BuhariImage 
Image captionRais Buhari, aliyeingia madarakani mwaka jana, aliahidi kukabili rushwa na ubadhirifu
Nigeria imetangaza kwamba itauza ndege mbili zinazotumiwa na rais wa nchi hiyo kama njia ya kupunguza matumizi mabaya ya pesa za umma.
Msemaji wa Rais Muhammadu Buhari, Garba Shehu, amesema ndege hizo mbili kati ya 10 zinazotumiwa na rais wa nchi hiyo zitauzwa kama sehemu ya kupunguza 'ubadhirifu' wa serikalini.
Serikali imeweka tangazo magazetini kwamba inauza ndege hizo, moja aina ya Falcon 7X na nyingine Hawker 4000.
  • Rais Buhari awataka Wanigeria wabadili tabia
Bw Shehu amesema Rais Buhari ndiye aliyeidhinisha matangazo hayo.
Ameongeza kwamba baadhi ya ndege nyingine za rais zitakabidhiwa jeshi la wanahewa la nchi hiyo.

BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU

HII NI MO DESIGN

Post a Comment

Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.

CodeNirvana
© Copyright MO Design
Back To Top