Akiongea na MO Design Ommy Janja Amesema anaamini kuwa ngoma hii ndio itakayomuweka pazuri zaidi katika ulimwengu wa mziki, ukiachana na ngoma yake ya kwanza kabisa iliyokuwa ikijulikana kwa jina la "MANENO MANENO SOO"
Ommy janja ameiambia MO Design kuwa sasa amekuja kupambana vikali na wakongwe wake kama akina Diamond na Ally kiba ambao ndio wameshikili game la mziki wa bongo flava kwa sasa, kwani anaamini kupitia kipaji chake naye atafikia hapo walipo.
CHEKI VIDEO
Lakini pia Chaka ambaye ni mshirika mwenzie Ommy, aliiambia MO Design kuwa, hakuna kukata tamaa na mapambano yanaendelea, akajaribu kutoa methali ya kwamba "WAO WAWEZE WANA NINI NA SISI TUSHINDWE TUNA NINI?,
Hapa alikuwa akimaanisha kuwa hao wanaoshikilia Gamu kwa sasa wana nini? kwani hata wao uwezo wanao na wataweza tu, Chaka Mlingula anatamba kwa sasa na kibao chake kiitwacho "SIDHANI KAMA NTAPENDA" Ambayo ipikwenye mitandao yote katika mfumo wa Audio na Video.
BOFYA HAPA KWA KUJIUNGA NASI MOJA KWA MOJA NA LIKE PAGE YETU
HII NI MO DESIGN
Post a Comment
Tafadhali, Usitumie lugha ya matusi! Maoni yako ni ya muhimu sana kwetu.